Timu ya Manchester United ya
England inataraji kumkosa mshambuliaji wake Robin van Persie mwanzoni mwa msimu mpya wa ligi
ambaye amerefushiwa muda wa mapumziko
baada ya kuwepo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi.
Kocha mkuu wa Manchester
United Louis van Gaal amesema mchezaji huyo ambaye bado yupo mapzikoni
anataraji kuanza mazoezi kesho jumatatu hivyo atatakiwa kuwa na muda mrefu wa
kujifua zaidi.
Van Gaal ambaye alikuwa na
kikosi cha timu ya taifa Uholanzi kilichoshika nafasi ya tatu kwenye kombe la
dunia zilizomalizika mwezi uliopita nchini Brazil amesema Van Persie hatocheza
mchezo wowote wa kujiandaa na msimu mpya utakaoanza katikakati ya mwezi huu.
United ambayo inataraji
kukata utepe wa ligi kuu ya England na Swansea City tarehe 16 ya mwezi huu
kwenye uwanja wake wa Old Traford
imeendelea kufanya vyema katika michezo yake ya majaribio nchini
Marekani baada ya jana kuifunga Real Madrid magoli 3 kwa1.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment