Timu ya soka ya Liverpool ya nchini
England imeendelea kuimarisha kikosi chake katika msimu huu wa usajili baada ya
kufanikiwa kumsajili kwa mkopo mlinzi wa pembeni kutoka kwa mabingwa wa ligi
kuu ya Hispania Atletico Madrid Javier Manquillo.
Manquillo mwenye umri wa miaka 20
yupo katika kikosi cha timu ya taifa ya Hispania ya vijana wenye umri wa miaka ishirini
mara baada ya kukamilisha uhamisho huo amesema anajisikia furaha kujiunga na
vijogoo hao wa Anfield.
Raia huyo wa Hispania amebainisha
kuwa anaamini Liverpool ni mmoja ya vilabu vikubwa barani Ulaya ambayo kila
mchezaji anatamani kuichezea hivyo atahakikisha anaonyesha kipaji chake.
Manquillo anakuwa mchezaji wa saba
kusajiliwa na kocha Brandan Rodgers msimu huu akiungana na Rickie Lambert, Adam
Lallana, Emre Can, Lazar Markovic, Dejan Lovren na Divock Origi.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment