kikosi cha Manchester United.
Mabingwa mara 20 wa ligi kuu
ya England timu ya Manchester United imefikia makubaliano na kampuni ya Adidas
kwaajili ya kutengeneza vifaa vyao vya michezo kwa mkataba wa miaka 10.
Taarifa kutoka katika tovuti
ya timu hiyo kongwe barani Ulaya na dunia kwa ujumla imethibitisha uwepo wa
makubaliano hayo ambapo udhamini huo ni wa thamani ya paundi milioni mia saba
na hamsini na unataraji kuanza msimu wa 2015/2016.
Udhamini huo umevunja rekodi
ya udhamini uliopita wa kampuni ya Nike ambao ulimalizika mwezi wa nne mwaka
huu na makubaliano ya kampuni hiyo ya Nike kutengeneza vifaa vya Manchester
United yanaishia mwezi huu wa saba.
Wakati huohuo kocha mpya
wa Manchestwer United Louis Van Gaal
anataraji kuanza kazi ya kuifundisha timu jumatano ya wiki hii baada ya kumalizika
kwa fainali za kombe la dunia ambapo kocha huyo ameeisaidia Uholanzi kushika
nafasi ya tatu.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment