Shirikisho
la Soka Duniani-FIFA limeitoza timu ya taifa ya Argentina faini ya dola 336,000 kwa kushindwa
kupeleka wachezaji katika mikutano minne ya wanahabari katika michuano ya Kombe
la Dunia.
Kamati
ya nidhamu ya FIFA imedai kuwa Argentina wamekiuka taratibu za vyombo vya
habari na masoko katika mikutano ya kabla ya mchezo kuanza kwenye michezo dhidi
ya Nigeria, Uswis, Ubelgiji na Uholanzi ambayo kocha pekee alikuwa anafika bila
mchezaji ikiwa ni kinyume na sheria za soka.
Argentina
watavaana na Ujerumani katika fainali ya michuano hiyo hapo kesho, lakini mpaka
hivi sasa hawajatoa kauli yoyote ya kama wanakubali au kukata rufani kutokana
na adhabu hiyo waliyopewa.
Hata
hivyo michuano ya kombe la dunia leo inaendelea nchini Brazil,ambapo wenyeji wa
michuano hiyo watakabiliana na Uholanzi ili kumtafuta mshindi wa tatu.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment