Vahid Halilhodzicakitoa maelekezo kwa nyota wa Algeria.
Timu ya soka ya Trabzonspor inayoshiriki
ligi kuu ya Uturuki imemteua aliyekuwa
kocha wa timu ya taifa ya Algeria Vahid Halilhodzic kuwa kocha wao mkuu.
Vahid mwenye umri wa miaka 61
aliiongoza vyema Algeria nakufikia hatua ya robo fainali kwenye michuano ya
kombe la dunia inayofikia tamati usiku huu nchini Brazil kwakuchezwa mchezo wa
fainali baina ya Argentina na Ujerumani.
Kocha huyo ambaye alijiuzulu mara
baada ya Algeria kuondoshwa na Ujerumani kwenye hatua ya robo fainali ya michuano ya
kombe la dunia hii ni mara yake ya pili kuinoa timu hiyo baada ya kuifundisha
mwaka 2005.
Hata hivyo kocha huyo
ambaye mkataba wake haujawekwa wazi ni wa muda gani amewahi kuvifundisha mataifa
mbalimbali ikiweno Croatia, France, Ivory Coast, Morocco na Saudi Arabia.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment