Wakati shirikisho la soka nchini Ivory Coast likitarajia
kumtangaza kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo,
Kocha Mfaransa Herve Renard ametajwa katika orodha ya mwisho ya kuwania
nafasi ya kukinoa kikosi hicho.
Orodha hiyo imetolewa na Shirikisho la Soka la nchi hiyo mwishoni
mwa wiki iliyopita ambapo makocha watatu wametajwa huku mshindi wa nafasi hiyo akitarajiwa
kutangazwa mwishoni mwa mwezi huu wa julai.
Renard ambaye aliiongoza timu ya taifa ya Zambia maarufu kama
Chipolopolo kushinda kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2012 anakabiliwa na
upinzani mkubwa kutoka kwa Mfaransa mwenzake Frederic Antonetti ambaye ameifundisha
Rennes.
Hata hivyo kocha wa zamani wa Sporting Lisbon na Benfica Jose
Manuel De Jesus wa Ureno ni miongoni mwa makocha wa wanaotarajiwa kuhojiwa na
kamati ya utendaji ya shirikisho hilo kabla ya uamuzi wa mwisho.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment