Baada ya Brazil kupokea kipigo cha
magoli 3 kwa 0 mbele ya Uholanzi usiku wa kuamkia leo kwenye mchezo wa kutafuta
mshindi wa tatu katika fainali za kombe la dunia kocha Luiz Flipe
Scolari amesema hatima yake ipo mikononi mwa
FA ya nchi hiyo.
Kocha huyo mwenye umri wa wa miaka 65 amesema mkataba wake unamalizika
mara baada ya kuisha kwa fainali za kombe la dunia lakini kulikuwa
kunamapendekezo ya kuendelea na kazi kama itawezekana.
Scolari ambaye aliiongoza Brazil
kushinda kombe la dunia mwaka 2002 amesema suala la kuendelea na kibarua cha
kuifundisha timu hiyo lipo mikononi mwa raisi wa shirikisho la soka la Brazil
na bodi yake nay eye atawasilisha taarifa yake ya mashindano mezani kwao.
Mchezo wa usiku wakuamkia leo ulikuwa wapili kufungwa
mfululizo baada ya jumanne ya wiki hii kufungwa magoli 7 kwa 1 na Ujerumani
katika hatua ya nusu fainali huo ukiwa ni mchezo wa kwanza Brazil kupoteza
nyumbani baada ya miaka 39 kupita.
Scolari akitoa maelekezo kwa Marcelo.
Matokeo ya usiku wa kuamkia leo ya
kufungwa michezo miwili mfululizo yamefikia rekodi ya mwaka 1940 ambapo Brazil ilipoteza michezo miwili
mfululizo kwenye ardhi ya nyumbani.
Katika
fainali za mwaka huu za kombe la dunia Brazil imeshinda michezo mitatu,kufungwa
miwili na kutoka sare mara mbili nakisha kushinda kwa mikwaju ya penalty dhifi
ya Chile.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment