Mlinzi wa klabu ya Manchester United, Rafael Da silva amerejea
nchini Uingereza kwa ajili ya matibabu kutokana na kuumia nyonga akiwa ziarani
nchini Marekani.
Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil aliumia wakati wa mazoezi jijini
Denver kuelekea katika mchezo wa
kirafiki walioshinda magoli matatu kwa
mawili dhidi ya AS Roma.
Rafael
kuna uwezekano asicheze tena michezo ya kujipima nguvu kabla ya kuanza kwa
msimu mpya wa ligi kuu England inayotarajiwa kuanza mwezi ujao huku kurejea kwake nyumbani kunampa matumaini ya
kupona haraka.
Manchester United itafungua pazia la Ligi Kuu England mwezi ujao kwa
kucheza na Swansea City katika Uwanja wa Old Trafford Agosti 16 mwaka huu.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment