Louis Van Gaal.
Kocha mpya wa timu ya
Manchester United Louis Van Gaal amewasili leo mjini Manchester tayari
kwakuanza kazi ya kuwanoa mabingwa wao mara 20 wa ligi kuu ya England.
Akiwa katika siku yake ya
kwanza Van Gaal mwenye umri wa miaka 62 amewasili kwenye uwanja wa mazoezi wa
Carrington ambao unatumiwa na Manchester United.
Van Gaal ambaye ameisaidia
Uholanzi kushika nafasi ya tatu kwenye kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil mchezo wake wa kwanza akiwa kocha wa Man
United utakuwa dhidi ya Valencia tarehe 12 ya mwezi ujao hili likiwa pambano la
kirafiki.
Kocha huyo kibarua chake cha
kwanza katika ligi kuu ya England ataikabili Swansea City tarehe 16 ya mwezi
ujao na baada ya Man United kufanya usajili wa Luke Show na Herrera timu hiyo
inawawinda Angel Di Maria na kiungo Arturo
Vidal wa Juventus.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment