Massimiliano Allegri
Mabingwa wa ligi kuu ya Italia Juventus wanataraji kumteua kocha wa zamani wa AC Milan Massimiliano Allegri kuchukua nafasi ya Antonio Conte
aliyejiuzulu hapo jana.
Imeelezwa kuwa Allegri
amefikia makubaliano na uongozi wa Juventus wa kuifundisha timu hiyo kwa
mkataba wa miaka miwili na uteuzi huo unataraji kutangazwa rasmi wakati wowote
kutoka sasa.
Uongozi wa Juve chini ya
rais wake Andrea Agnelli asubuhi ya leo jumatano umfanya mazungumzo na Allegri
nafikia makubaliano ya kumpa kocha huyo mkataba wa miaka miwili wenye thamani
ya Euro milioni 2 kwa msimu pamoja na bonasi mbalimbali.
Allegri ambaye amekuwa hana kazi tangu atimuliwe na AC Milan mwezi wa kwanza mwaka huu anatarajiwa kuanza kazi kesho alhamisi
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment