Thursday, July 31, 2014
NADAL KUKAA NJE WIKI MBILI HADI TATU.
Rafael Nadal.
Mcheza Tenisi Rafael Nadal anataraji kukaa nje ya uwanja kwa majuma matatu baada ya kuuumia kifundo cha kiganja wakati akifanya mazoezi jumanne ya wiki hii.
Kuumia kwa mchezaji huyo anayeshika nafasi ya pili kwa ubora wa Tenisi duniani kumekuja ikiwa ni majuma kadhaa kabla ya kuanza kwa mashindano ya wazi ya marekani yanayotaraji kufanyika mjini New York Marekani.
Nadal mwenye umri wa miaka 28 kwasasa atashindwa kutetea mataji yake ya michuano ya Toronto na Cincinnati mwaka huu huku ikielezwa atakuwa tayari kurejea uwanjani kwenye michuano ya wazi ya Marekani inayoanza tarehe 25 ya mwezi wa nane.
Mchezaji huyo amethibitisha kuwa ameumia kifundo cha mkono wake wa kulia wakati akiwa mazoezini na anataraji kupatiwa matibabu na madaktari wake yatakayomfanya atumie majuma mawili hadi matatu ili kupona.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment