Ronaldinho Gaucho
Kocha mkuu wa timu ya
Atletico Mineiro ya nchini Brazil Levir Culpi amethibitisha kuwa wamevunja mkataba na
mshambuliaji mkongwe wa kikosi hicho
Ronaldinho Gaucho ambaye amewahi kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia.
Ronadinho ambaye alisaini
mkataba mpya wa mwaka mmoja mwezi wa kwanza mwaka huu licha ya kwamba alikuwa
na nia ya kuhamia timu ya Besiktas ya Uturuki.
Kocha wa Mineiro mbali na
kumshukuru nyota huyo wa zamani wa Fc Barcelona na timu ya taifa ya Brazil
kesho jumatano Ronaldinho anatarajiwa kuwa na mkutano na waandishi wa habari
kutangaza matarajio yake ya baadae.
Ronaldinho ambae alijiunga na Atletico Mineiro mwezi wa sita
mwaka 2012 baada ya kuachana na timu ya Flamengo licha ya kuhusishwa na
mipanggo ya kujiunga na Boca Junior inayosaka mrithi wa Juan Roman Riquelme pia
inaelezwa huenda akajiunga na ligi ya Marekani MLS.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment