Pages

Ads 468x60px

Friday, January 16, 2015

WAJUE CAPE VERDE KUELEKEA FAINALI ZA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA MWAKA HUU WA 2015.



                                Kikosi cha timu ya taifa ya Cape Verde.

Cape verde ni taifa lililopata uhuru wake kutoka kwa Ureno mwaka  1975.
Hiki ni kisiwa kidogo kilichopo katika bahari ya Atlantic chenye watu wapatao  498 897 (laki nne tisini na nane elfu,mia nane na tisini na saba).kwa takwimu za mwaka 2013.
Mji wake mkuu ni Praia .
Miongoni mwa miji mashuhuri katika taifa hili ni..Boa Vista,santa maria Cape verde mji mashuhuri kwa uvuvi wa samaki uliopo km 16 kutoka kusini mwa uwanja wa ndege wa Amílcar Cabral, miji miningine ni kama Pedra Lume salt crater, Olho Azul, Buracona na Fontana.
Lugha kuu ya raia wa taifa hili  ni Kireno.
Rais wa nchi hii ni ... Jorge Carlos de Almeida Fonseca aliyeingia madarakani sept 9 mwaka 2011 akichukua nafasi ya Pedro Verona Rodriguez Pires  aliekaa madarakani kuanzia march 22 mwaka 2001 hadi sept 9 mwaka 2011.

 Tangu ipate uhuru wake kutoka kwa Wareno mwaka 1975 nchi hii imeongozwa na marais wanne tuu ambao ni Aristides Maria Pereira julai 8 1975 hadi januari 1981,januari 1981 hasi march 22 mwaka 1991 na kumpisha  António Mascarenhas Monteiro, kuanzia 22 March 1991  hadi  22 March 2001 kisha Pedro Verona Rodrigues Pires  kupewa kijiti cha urais kuanzia 22 March 2001 hadi  9 September 2011 naye kumpa kijiti hicho cha urais  Jorge Carlos de Almeida Fonseca kuanzia 9 September 2011  ambaye yupo madarakani hadi  hivi sasa.
Timu ya soka ya taifa ya Cape verde inajulikana kwa jina la utani kama Blue Sharks yaani Papa buluu.wakijivunia samaki huyo anayepatikana kwa wingi katika bahari ya Atlantic.
Ni samaki mkubwa ambaye hupatikana katika bahari kubwa duniani na inaelezwa hufikia uzito mkubwa kabisa wa kg 391.
Cape verde inashika nafasi ya 40 katika ubora wa soka duniani katika takwimu zilizotolewa januari 18 mwaka huuwa 2015.
Nafasi ya juu kabisa iliyoshika nchi hii katika ubora wa soka duniani ni ya 27 na hii ilikuwa  february mwaka 2014 huku nafasi ya chini kabisha kushikwa na taifa hilo ni ya 182 ilikuwa ni April mwaka 2000.
 Kwamara ya kwanza Cape Verde kucheza mechi ya kimataifa ilikuwa mwaka 1978 ambapo hatahivyo tarehe na mwezi havikuwekwa wazi  walicheza na Angola na kufungwa goli 1 kwa 0.
Ushindi mkubwa iliyowahi kuupata Cape verde ni wa magoli 5 kwa 0 dhidi ya Equetorial Guinea march 28 mwaka 2009 na kipigo kikubwa walichowahi kukipata ni cha magoli 5 kwa 1 dhidi ya Senegal february 12 1981.
Pia vipigo vikubwa waliowahi kuvipata ni magoli 4 kwa 0 kutoka kwa  Ghana Octoba 8 mwaka 2005 pamoja na kipigo kama hicho walichokipata kutoka kwa Guinea september 9 mwaka 2007.
FAINALI ZA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA (AFCON).

Mashabiki wa soka nchini Cape Verde hawapo mbali na timu yao,hapa walikuwa nayo nchini Afrika kusini 2013.

 Mashabiki wa Cape Verde wakifanya yao nchini Afrika kusini katika fainali zilizopita ambapo timu yao ya taifa iliishishia robo fainali.


Mara ya kwanza kwa Cape verde kushiriki fainali hizi ni mwaka 2013 ambapo ilifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali  fainali zilizofanyika nchini Afrika ya kusini na Nigeria kutawazwa mabingwa baada ya kuifunga Burkinafaso goli 1 kwa 0.
Kinara wa magoli kwenye timu ya taifa ya Cape verde ni mchezaji Carlos Morais, Héldon Ramos mwenye magoli 10.
Kocha mkuu wa timu hiyo hivi sasa ni Rui Águas kwakirefu jina lake ni Jose Rui Lopes Aguas mzaliwa wa Lisbon Ureno na nyota wa zamani wa Benifica ya Ureno.
Nahodha wa timu hii ni  Marco Soares anyecheza nafasi ya kiungo akiichezea pia klabu ya AC Omonia ya nchini Cyprus.
Katika fainali za mwaka huu zinazofanyika nchini Guinea Cape Verde imepangwa kwenye kundi B lenye mataifa ya ZAMBIA,TUNISIA,na DR CONGO.
Je taifa hili changa kisoka litaendelea kuuteka umma wa Afrika kwenye fainali za mwaka huu wakiwa wanashiriki kwa mara ya pili?wapo wasio lipa nafasi taifa hili linalokua kwa kasi kisoka licha ya kutosheheni majina makubwa umaarufu kwao sio tija bali wanajivunia vipaji lukuki walivyobarikiwa Kama ...viungo Toni Varela,Nuno Rocha,Garry Rodriguez na Monteiro  Masedo ambaye ni fundi wa kupiga mipira kwa miguu yote huku safu ya ushambuliaji ikiongozwa na wakali kama ...Ryan Mendez, Jorge Djaniny na  Julio Tavares ambaye uzito wake wa kg 85 haumsumbui kufanya chochote kwenye lango la adui.
Hawa ndio  Cape Verde wenyeyewe wanajiita( Blue Sharks)yaani PAPA BLU.
Naamini mashabiki wa Cape verde kama ndugu yangu Luther Akyoo mtakuwa mmefarijika kwa historia fupi ya taifa hili changa kisoka lakini  ni moto wa kuotea mbali.

                                     Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment