Hatem Ben Arfa.
Shirikisho la soka duniani FIFA
limezuia uhamisho wa mshambuliaji hatem ben arfa kutoka Hull city kwenda katika
klabu ya nice inayoshiriki ligi kuu ya nchini ufaransa maarufu kama Ligi wani.
Ben Arfa raia wa ufaransa
amezuiwa kuhamia katika klabu hiyo ambayo ilitangaza kumpa mkataba wa miezi 18 lakini
FIFA imesema usajili huo upo kinyume na kanuni za usajili.
Shirikisho hilo imefafanua kuwa
sheria za usajili haziruhusu mchezaji kusajiliwa na vilabu viwili tofauti ndani
ya msimu mmoja pekee kama ilivyotokea
kwa Hatem ben arfa.
Nyota huyo mwenye mwenye umri
wa miaka 27 alikua akiitumikia hull city kwa mkopo akitokea Newcastle united
ambapo baada ya kumaliza muda wake na hull city Newcastle ilisitisha mkataba
wake.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment