Pages

Ads 468x60px

Saturday, January 17, 2015

WAFAHAMU SIMBA WA TERANGA A.K.A SENEGAL KUELEKEA AFCON 2015.



              Senegal,Simba wa Teranga waliojiandaa kurejesha heshima yao barani Afrika.

Senegal ilipata Uhuru wake mwaka 1960 ikiwa koloni la Ufaransa.
Kiongozi mkuu wa nchi ya Senegal ni RAIS na  hii ni baada ya katiba  ya taifa hilo  iliyopitishwa  mwaka 2001 ambapo  rais wa nchini hiyo huongoza kwa miaka mitano ndipo uchaguzi hufanyika.
Rais wa sasa wa Senegal ni Macky Sall aliyezaliwa mwaka 1961 na aliingia madarakani  April 2 mwaka 2012 akichukua nafasi ya Abdoulaye Wade aliingia madarakani  April 1 2000 akichukua mikoba ya rais wa wakati huo Abdou Diouf aliyeingia matarakani  January 1 mwaka 1981.
Tangu ipate uhuru wake kutoka kwa Ufaransa mwaka 1960 Senegal imeongozwa na marais wane tuu akiwemo huyu wasasa.
Rais wa kwanza ambaye ni baba wa taifa la Senegal ni Léopold Sédar Senghor aliyeongoza kwa miaka 20 tangu  sept 6 1960 hadi dec 31 1981, alizaliwa mwaka 1906 na kufariki dunia 2001 akiwa na umri wa miaka 95.
 Nchi hii inapatikana magharibi mwa bara la Afrika  na mjini mkuu wake ni Dakar mji unaotajwa kuwa na wakazi milioni 2.45 wanaoishi jijini humo.
Hadi dec mwaka jana taifa hili  linakadiriwa kuwa na watu wapatao milioni 14 laki 786 mia 504,wanaume wakiwa milioni 7333 705 sawa na 49.6%   ya wananchi wote huku wanawake wakiwa milioni 7452 801 sawa na 50.4%.
Lugha kuu ya taifa la Senegal ni Kifaransa.
Miongoni mwa miji mashuhuri nchini Senegal mbali na jiji la Dakar  ni.. Sant Louis, Ziguinchor na M'Bour.
Uchumi wa wananchi ya Senegal  unategemea Uvuvi,kilimo cha karanga,utalii na madini aina ya phosphates, na asilimia kubwa ya wananchi wa taifa hili ni wakulima.
Timu ya taifa ya Senegal inajulikana kama SIMBA WA TERANGA kwa jina la utani .
Mara ya kwanza kucheza mchezo wa kimataifa kwa timu hii ilikuwa dhidi ya British Gambia mwaka 1959 wakati huo Senegal ikijulikana kama  French Senegal.
Katika mchezo huo Senegal ilishinda magoli 2 kwa 1 dhidi ya British Gambia ambayo kwasasa inajulikana kama Gambia.

Ushindi mkubwa iliyowahi kuupata Senegal ni wa magoli 7 kwa 0 dhidi ya Mouritius ilikuwa oct 9 mwaka 2010.
Kipigo kikubwa ilichowahi kukipata timu ya taifa ya Senegal au Simba wa Teranga ni cha magoli 5 kwa 0 kutoka kwa Guinea march 6 mwaka 1966.
Senegal imeshiriki kombe la dunia mara moja tuu  mwaka 2002 na kufikia hatua ya robo fainali wakati huo kikosi hicho kikiwa chini ya kocha Bruno Metsu na kuongozwa na nahodha wa wakati huo Alhadji Diof nyota wa zamani wa vilabu mbalimbali barani Ulaya ikiwemo Liveroop.
Bila shaka wengi mtaikumbuka Senegali hii ambayo iliushangaza Ulimwengu kwakuifurusha Ufaransa ya Zinedine Zidane  goli 1 kwa 0 na kuwa talk of the World.
Baada ya ukali huo wa 2002 Senegal ikapotea kiasi cha wengi kuhoji kulikoni?ikawa hivo baadae aliyekuwa kocha wa Senegal wakati huo Bruno Metsu akaondoka na taarifa za kushtua zikajiri  October 14 2013 kwamba amefariki dunia  katika kijiji cha Coudekerque kilichopo nchini Ufaransa .
Daima atakumbukwa na mashabiki wengi wa Senegal kwa mchango wake alioutoa kwa timu yao ya taifa.
 Kwasasa Senegal inashika nafasi ya 35 kwenye ubora wa soka duniani kwenye takwimu zilizotolewa January 8 mwaka huu.
Nafasi ya juu kuwahi kushika katika ubora wa soka duniani ni ya 26 na hii ilikuwa juni 2004 na nafasi ya chini zaidi kuwahi kushika nchi hii katika ubora huo wa soka duniani ni ya 99 mwezi juni mwaka 2013.
Kocha mkuu wa sasa wa timu ya taifa ya Senegal ni Alain Giresse akisaidiwa na kocha msaidizi Aliou Cisse na nahodha wa kikosi hichi kwasasa ni Bouna Condoul ambaye hucheza nafasi ya Golini ya Mlindamlango.
FAINALI ZA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA.
Senegal al maarufu Simba wa Teranga imeshiriki kombe la mataifa ya Afrika AFCON mara 12.
Mara ya kwanza ilikuwa 1965.
Hatua nzuri iliyowahi kufikia  kwenye fainali hizi ni kushika nafasi ya 2 katika fainali za mwaka 2002  zilizofanyika nchini MALI na ubingwa kunyakuliwa na CAMEROON huu ukiwa ni ubingwa wa 4 kwao.
 Katika fainali za AFCON mwaka huu Senegal ni miongoni mwa mataifa yatakayoshiriki huko nchini Guinea ikiwa na muonekano wa tofauti kabisa na wengi walivyotarajia.
Wachezaji wenye majina kama Demba Ba  wameaachwa kwenye kikosi hicho na badala yake chipkizi wamesheheni katika kikosi hichi chini ya kocha mkuu Alain Giresse.
Wapo katika kundi linaloaminika kuwa ni la kifo,kundi C lenye mataifa kama Ghana,Algeria,na Afrika ya kusini.
Pamoja na kuwa kwenye kundi la kifo Simba hawa wa Teranga huenda wakarejesha heshima yao iliyopotea tangu mwaka 2002 walipotinga robo fainali ya kombe la dunia  kutokana kocha wa sasa kukisuka upya kikosi hicho huku kikisheheni nyota wengi wanaosakata soka barani Ulaya hususani Ufaransa ambapo ni Koloni lao.
Hebu angalia safu ya hii ya ushambuliaji wa Simba hawa wa Teranga inayoundwa na nyota wanaotamba katika ligi kuu mbalimbali barani Ulaya hususani  Uingereza hivi sasa Diafra Sakho (West Ham, England), Mame Birame Diouf (Stoke, England), Sadio Mané (Southampton, England), Moussa Sow (Fenerbahçe, Turkey), Papiss Demba Cissé (Newcastle, England), Henri Saivet (Bordeaux, France), Dame Ndoye (Lokomotiv, Russia), Moussa Konaté (FC Sion, Switzerland)
Mimi nakuachia wewe utafakari  lakini sidhani kama Simba wateranga wanaenda kutalii nchini Guinea mwaka huu bali wanaenda kuweka historia nyingine mhimu katika soka la barani Afrika hivi sasa.
                                          Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment