Victor Wanyama akiwa amelala baada ya kuumia.
Klabu ya soka ya
Southampton ya Uingereza itamkosa kwa majuma 6 nyota wake raia wa Kenya victor
wanyama baada ya kuumia kwenye mchezo wa kufuzu mzunguko wa 4 wa michuano ya FA.
Kocha mkuu wa klabu ya hiyo Ronald Koeman amethibitisha
kuwa wanyama ameumia nyama za paja hivyo kwenye mchezo dhidi ya
Ipswich town hivyo atakuwa nje ya uwanja kwa muda huo .
Kutokana na maumivu hayo
wanyama mwenye umri wa miaka 25 atakosa michezo ya timu yake dhidi ya
Liverpool,Newcastle united ,Swansea city ,QPR pamoja na west ham United.
Nyota huyo ambaye amekuwa
mchezaji muhimu katika kikosi ya koeman akifanikiwa kuanza kwenye michezo 24
,anaungana na nyota wengine Morgan
Schneiderlin na Toby Alderweireld ambao pio majeruhi.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment