Keylor Navas.
Timu ya soka ya Real Madrid ya Hispania imekamilisha usajili wa mlindamlango Keylor Navas kutoka Levante kwa mkataba wa miaka sita ya kuwa Santiago Bernabeu.
Taarifa zilizothibitishwa na tovuti ya Real Madrid imeeleza kufikiwa kwa makubaliano baiana ya timu hizo mbili na sasa ni mchezaji halali wa mabingwa hao wa Ulaya kwa upande wa vilabu.
Navas mwenye umri wa miaka 27 anataraji kutambulishwa rasmi katika timu ya Real Madrid kesho jumaane kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu mara baada ya kukamilisha vipimo vya afya.
Navas ambaye
ni raia wa Costa Rica aliisadia nchi yake kufanya vyema kwenye fainali za kombe
la dunia zilizomalizika mwezi uliopita nchini Brazil jambo lililovivutia vilabu
mbalimbali duniani ikiwemo Real Madrid iliyomsajili.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment