Xabi Alonso.
Mabingwa wa
ligi kuu ya Ujerumani Bayern Munich
wametangaza kufikia makubaliano na Real
Madrid ya Hispania juu ya kumsajili
kiungo Xabi Alonso na leo
alhamisi mchezaji huyo anatarajiwa kuwasili Ujerumani kufanyiwa vipimo vya
Afya.
Mabingwa hao
wa Bundesiliga wamelazimika kusaka mchezaji wa nafasi ya kiungo baada ya kuumia kwa Javi Martinenz,Bastian
Schweinsteiger na Thiago Alcantara hivyo
wanaamini Alonso mwenye umri wa miaka 32 anaweza kuwafaa kwa hivi sasa.
Taarifa za
vilabu hivyo kufikia makubaliano ya kuuziana mchezaji huyo wa zamani wa
Liverpool zimethibitishwa na mmoja wa
wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa Bavarians Jan-Christian Dreesen kwenye
mkutano wake na waandishi wa habari.
Mjumbe huyo wa Bayern
amethibitisha kwakuesema Alonzo ambaye
amecheza michezo zaidi ya 200 akiwa Santiago Bernabeu mara baada ya kufanyiwa
vipimo leo mjini Munich atasaini mkataba
na kutua rasmi Allianz Arena.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment