Pages

Ads 468x60px

Wednesday, August 20, 2014

ELMEREKH YAENDELEZA UNDAVA KWA TIMU ZA TANZANIA YAIFUMUA AZAM FC NAKUIFUNGASHA VIRAGO KAGAME 2014.



                         Kikosi cha mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Azam fc.

Mabingwa wa ligi kuu ya soka Tanzania bara timu ya Azam fc ya jijini Daresalaam leo imeiaga michuano ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati maarufu kama Kagame baada ya kutolewa kwa changamoto ya mikwaju ya Penalts 4 kwa 3 na Elmerekh ya Sudani.
Katika mchezo huo wa robo fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Nyamirambo Kigali Rwanda Azam fc ilitoka sare ya kutofungana na Elmerekh  ndipo changamoto ya mikwaju ya matuta kutumika kumsaka mshindi.
Katika changamoto hiyo ya Matuta Azam fc ilijikuta ikiambulia magoli 3 yaliyofungwa na wachezaji Agrey Moris,Didier Kavumbagu na Ereasto Nyoni huku mkwaju wa beki wa kupanda na kushuka Shomari Kapombe ukigonga mtambaa panya kabla ya Leonel Saint- Preux shuti lake kudakwa na mlindamlango wa Elmerekh.
Mlinda mlango wa Azam fc Mwadini Ally Mwadin alifanikiwa kupangua mkwaju mmoja wa Penalti kisha kufungwa mikwaju minne kati ya mitano iliyopigwa na wachezaji wa Elmerekh.
Wakati Azam fc ikijiandaa kurejea nyumbani baada ya kuiga michuano hiyo ya mwaka huu ambapo mabingwa hao wa ligi kuu ya soka Tanzania bara walipata bahati kufuatia Yanga kuenguliwa na CECAFA Elmerekh imeungana na Polisi pamoja na APR zote za nchini Rwanda kutinga nusu fainali.
Robo fainali ya pili hii leo ni baina ya KCCA ya Uganda na Atlabara juba ya Sudani kusini.
                             
                        Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment