Pages

Ads 468x60px

Sunday, August 24, 2014

UWANJA WA TIMU YA SHAKTAR DONETSK WALIPULIWA NA MABOMU NCHINI UKRAIN.



                Uwanja wa Donbass Arena baada ya kulipuliwa na mabomu.

Ghasia nchini Ukrain zimeendelea kusababisha maafa hata kwenye miundombinu ya michezo baada ya mabomu mawili kuharibu  uwanja wa Donbass Arena unaomilikiwa na klabu ya Shaktar Donetsk  inayoshiriki ligi kuu ya huko.
Mabomu hayo yaliyolipuka jana  licha ya kutojeruhi mtu yeyote  yameharibu  vifaa vya mawasiliano vilivyoko kwenye uwanja huo ambao ulitumika katika  nusu fainali ya mataifa ya Ulaya mwaka 2012  baina ya Hispania na Ureno.
Uwanja huo pia ulitumiwa na Shaktar Donetsk  walipokuwa wanacheza na Manchester United mwezi wa kumi mwaka jana kwenye michuano ya klabu bingwa Ulaya ambapo timu hizo zilitoka sare ya kufungana goli 1 kwa 1.
Tayari timu ya Shaktar Donetsk  imeshahama kwenye  mji wa Donetsk  yalipo  makazi yao na kuhamia mji wa Lviv ambapo michezo yao  ya ligi  ikiwemo ile ya klabu bingwa Ulaya itachezwa  huko kutokana na machafuko yanayoendelea Ukrain.
            Uwanja wa Donbass Arena unavyonekana dani kabla ya kulipuliwa na mabomu


     Uwanja wa Donbass Arena unavyonekana  kwa nje kabla ya kulipuliwa na mabomu
                            Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment