Balotelli akikunjana na aliyekuwa kocha wa manchester City Roberto Mancin enzi hizo 2012
Klabu ya Liverpool ya England imeripotiwa kufikia makubaliano na AC Milan juu ya kumsajili mshambuliaji Mario Balotelli kwa uhamisho wa paundi milioni 16 tayari kwa kumnyakua mtukutu huyo raia wa Italia.
Balotelli ambaye alijiunga na Milan kwa ada ya paundi milioni 19 akitokea Manchester City amekuwa kati ya wachezaji wanaosakwa na kwa udi na uvumba kwa siku za hivi karibuni na kocha wa Liverpool Brendan Rogers ambaye anataka kuiongeza nguvu safu yake ya ushambuliaji baada ya kuondoka kwa Luis Suarez alihamia Fc Barcelona.
Kwasasa imeelezwa Balotelli yupo kwenye makubaliano binafsi na uongozi wa Liverpool na kama yatakamilika atakamilisha uhamisho huo mara moja.
Tangu ajiunge na AC Milan Balotelli amefunga magoli 30 katika michezo 54 aliyocheza katika ligi kuu ya Italia maarufu kama Serie A.
Tarifa za Liverpool kuwa kwenye makubaliano na Milan juu ya kuuziana mchezaji huyo zimekuja wakati Liver ikijiandaa kuikabili Machester City juamatatu ijayo katika mfululizo wa ligi kuu ya England iliyoanza jumamosi iliyopita.
Tovuti ya klabu ya AC Milan imethibitisha Balotelli kuondoka Milan leo na kuagana na wachezaji wenzake sambamba na kuwaaga wfanyakazi waliyopo katika ofisi za Milan
Balotelli alijiunga na Manchester City mwezi Augost kutoka Inter Milan ya Italia kwa uhamisho wa paund milioni 24 na kufunga magoli 30 katika michezo 80 nakuisaidia Man City kunyakua taji la kwanza la ligi kuu ya England chini ya kocha Roberto Mancin ambaye baade alitimuliwa.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment