Miroslav Klose akiwa na kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ujeruman Joachim Low.
Mshambuliaji
wa Lazio ya Italia na timu ya taifa ya Ujeruman Miroslav Klose ametangaza rasmi
kustaafu kitumikia timu yake ya taifa
akiwa na umri wa miaka 36.
Klose ambaye
katika fainali za kombe la dunia mwaka huu ameisaidia Ujeruman kutwaa ubingwa
kwenye fainali zilizofanyika nchini Brazil amestaafu akiwa anashikilia rekodi
ya kuwa mfungaji wa muda wote wa fainali
hizo kwakufikisha magoli 16.
Mkongwe huyo
ambaye hatosahaulika kwenye soka la kimataifa kutokana na uhodari wake aliokuwa
nao wa kufunga magoli ya kishwa kwenye fainali za mwaka huu alifanikiwa kufunga
magoli mawili katika michezo mitano
aliyocheza.
Akizungumzia
uamuzi wake wa kustaafu Klose amesema anashukuru kutimiza ndoto ya kutwaa kombe
la dunia katika maisha yake ya soka na hakuna njia nyingine ya kustafu soka
kama sasa ilikuwapisha vijana.
Nyota huyo amesema katika maisha yake ya soka kuitumikia timu ya taifa lilikuwa jambo la kwanza na alikuwa hafikirii kuweka rekodi bali kuchezwa kwa moyo wake wote kwenye timu ya taifa na kazi yake ilikuwa kufunga magoli.
Nyota huyo amesema katika maisha yake ya soka kuitumikia timu ya taifa lilikuwa jambo la kwanza na alikuwa hafikirii kuweka rekodi bali kuchezwa kwa moyo wake wote kwenye timu ya taifa na kazi yake ilikuwa kufunga magoli.
Miroslav Klose akiwa ameshikilia kombe la dunia mwezi jana nchini Brazil
Klose alicheza mchezo wake wa kwanza kwenye timu ya taifa ya Ujerumani mwezi wa 3 mwaka 2001 ambapo Ujerumani iliifunga Albania magoli 2 kwa 1 na alifunga goli la ushindi dakika 19 klaby ya pambano hilo kumalizika.
Klose alicheza mchezo wake wa kwanza kwenye timu ya taifa ya Ujerumani mwezi wa 3 mwaka 2001 ambapo Ujerumani iliifunga Albania magoli 2 kwa 1 na alifunga goli la ushindi dakika 19 klaby ya pambano hilo kumalizika.
Hadi na
tundika daluga mkongwe huyo amecheza michezo 137 akiwa na kikosi cha timu ya
taifa ya Ujeruman akiwa nyuma ya mkongwe Lothar Matthaus aliyecheza michezo
150.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment