Arsene Wenger.
Kocha mkuu wa timu ya Arsenal
mfaransa Arsene Wenger amesema anampango ya kutafuta mlinzi wakati atakaechukua
nafasi ya Thomas Vermaelen ambaye amesajiliwa na vigogo vya soka nchini
Hispania klabu ya Fc Barcelona.
Licha ya uwezo mzuri
ulioonyeshwa na chipkizi Calum Chambers jana jumapili kwenye mchezo wa ngao ya
jamii ambapo Arsenal ilifanikiwa kushinda magoli 3 kwa 0 ddhidi ya Manchester City kocha Arsene Wenger
amesema atatafuta mbadala wa Vermaelen.
Japo kocha huyo amekiri kuwa
sio jambo rahisi kupata mlinzi mzuri kwa haraka lakini kama itawezekana kufanya
usajili kipindi hiki atahakikisha nafanya hivyo licha ya kuridhishwa na uwezo
wa Chambers hapo jana.
Arsenal ambaye imeonyesha uwezo
mzuri hapo jana kwakuwafunga mabingwa wa lighi kuu ya England kocha mkuu ambaye
amedumu na kikosi hicho muda mrefu amesema kwasasa wachezaji wote wapo tayari
kwaajili ya msimu mpya unaoanza mwishoni mwa juma hili.
Mkule.blogsports.com
No comments:
Post a Comment