Klabu
ya Manchester United ya England imefikia makubaliano ya kumsajili mlinzi wa
timu ya Sporting Lisbon ya Ureno Marcos Rojo kwa ada ya Euro milioni 20 sambamba
na kumtoa kwa mkopo wa muda mrefu mchezaji Luis Nani.
Rojo
mwenye umri wa miaka 24 anatarajiwa kuwasili Old Traford baada ya makubaliano
hayo kufikiwa na klabu zote mbili na raia huyo wa Argentina atarudi Ureno
kwaajili ya kuwaaga wachezaji wenzake wa Sporting na mashabikiwa timu hiyo.
Kocha wa Man United Louis Van Gaal ametoa sababu ya kusajili
mlinzi huyo kwakusema anauwezo mkubwa wa
kucheza mfumo anayoutumia baada ya kufungwa na Swansea City magoli 2 kwa 1 katika
ligi kuu ya England siku ya jumamosi.
Katika mauzo ya mchezaji huyo
Sporting itailipa timu ya Spartak Moscow Euro milioni 5 ambayo aliichezea Rojo
na asilimia 75 itaenda kwa taasisi ya Doyen Sport ambayo inamiliki hati za
kiuchumi za mchezaji hivyo Sporting haitaambulia chochote.
Mkule.blogsport.com.
No comments:
Post a Comment