kikosi cha Atletico madrid kikishangilia ubingwa wa Spanish super cup.
Timu ya soka ya Atletico Madrid imefanikiwa kuifunga Real Madrid goli 1 kwa 0 katika mchezo wa marejeano wa Spanish Super Cup uliochezwa usiku wa jana kwenye uwanja wa Vicente Calderon na kunyakua taji hiyo kwa jumla ya magoli 2 kwa 1 baada ya kutoka sare ya goli 1 kwa 1 kwenye mchezo wa awali.
Alikuwa ni mchezaji mpya wa Atletico Madrid Mario Mandzukic aliyewanyanyua mashabiki wa timu hiyo kwenye uwanja wao wa nyumbani aliyefunga bao hilo pekee na la ushindi kwa vijana wa Diego Semione ambao ni mabingwa wa La liga msimu uliopita.
Katika mchezo huo ambayo ulikuwa wa kuashiria kuanza kwa ligi kuu ya Hispania msimu huu wa 2014/2015 nyota mpya wa Real Madrid Jemes Rodriguez alipata nafasi mbili za wazi lakini guu lake halikulenga goli sawasawa na kuifanya timu yake kutoka uwanjani vichwa chini kwa kipigo hicho cha jumla ya magoli 2 kwa 1 ukijumuisha matokeo ya pambano la awali lililopigwa Santiago Bernabeu.
Mario Mandzukic ambaye alisajiliwa kwa Euro milioni 20 akitokea Bayern Munich alifunga goli hilo la pekee kwenye mchezo huo mapema katika dakika ya 2 baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Antoine Griezmann.
Pamoja na washambuliaji wa Real Madrid wakiongozwa na Jemes Rodriguez,Gareth Bale,Tony Kross na Karimu Benzema kuonyesha uwezo mkubwa ndani ya dimba la Vicente Calderon haikusaidia kuepuka kipigo hicho cha goli 1 kwa 0 kwani ngome ya Atletico Madrid ilionekana kuwa imara kuzima mashabulizi yote yaliyoelekezwa langoni mwao.
Mario Mandzukic akishangilia goli alilofunga kwenye mchezo wa jana usiku kati ya timu yake ya Atletico Madrid na Real Madri uwanja wa Vicente Calderon.
Wakati huohuo pazia la ligi kuu ya Hipania linataraji kufunguliwa rasmi leo kwa kuchezwa michezo ifuatayo:-
KESHO.AUG 24 2014.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment