Pages

Ads 468x60px

Saturday, August 23, 2014

TANZANIA ELEVEN HOI KWA WAKONGWE WA REAL MADRID YAPIGWA 3 KWA 1 KAMA WAMEVAA NDALA.



Mkongwe wa Real Madrid Luis Figo akiwatoka walinzi wa Tanzania Eleven jioni ya leo kwenye uwanja wa taifa jijini Daresalaam.

Timu ya soka ya Tanzania Eleven inayojumuisha wakongwe wa Tanzania waliowahi kung’ara na timu mbalimbali nchini pamoja na timu ya taifa leo imechezea kichapo cha magoli 3 kwa  1 kutoka kwa wakongwe wa Real Madrid ya Hispania kwenye pambano la kirafiki  liliochezwa uwanja wa taifa jijini Daresalaam.
Katika pambano hilo lilohudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mh.daktari Jakaya Kikwete hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana goli 1 kwa 1.
Kipindi cha pili pamoja na mabadiliko kadha a yaliyokuwa yakifanywa na kocha mkuu wa timu ya Tanzania Eleven Charles Bonifas Mkwasa na msaidizi wake Jamhuri Kiwelu Julio kikosi hicho kilishindwa kufua dafu mbele ya wakongwe wa Real Madrid waliokuwa wakiongozwa vyema na Luis Figo.
Katika pambano hilo magoli yote ya wakongwe wa Real Madrid yalitiwa kambani na mchezaji De la Red kunako dakika za 10,81 na 88  goli la dkk 81 lilikuwa la mkwaju wa penalt baada ya mfungaji huo kuchezwa madhambi ndani ya maguu 18 ya mtu mzima.
Pao pekee la Tanzania Eleven lilipatikana dkk ya 45 ambapo mkongwe wa Real Madrid Roberto Rojas alijifunga katika harakati za kuokoa mpira wa kona uliochongwa na nahodha wa zamani wa Taifa Stars na kocha wa sasa wa mtibwa sukari Meck Mexime.
 Hadi dakika 90 zinamalizika wakongwe wa Real Madrid 3 tanzania Eleven goli 1.
Miongoni mwa nyota wa Tanzania waliocheza hii leo ni ..Mohamed Mwameja amabye baadae nafasi yake ilichukuliwa na Piter Manyika,Meck Mexime,Kalimangonga Ongala,Habibu Kondo,Shadrack Nsajigwa, Shabn Ramadhani ,Madaraka Suleiman na Athman China.
Baada ya pambano hilo usimu huu wachezaji wote wanataraji kula shakula cha pamoja na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mh.Jakaya Kikwete Ikulu jiji Daresalaam.

                        Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment