Timu ya Benfica ya nchini Ureno
imethibitisha kumsajili mlinda mlango Julio Cesar kwa uhamisho huru baada ya
klabu ya QPR kukatisha mkataba wake wa miaka miwili uliokuwa umesalia kwa
makubaliano ya pamoja.
Nyota huyo wa zamani wa timu ya taifa ya
Brzail amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Benfica inaotumia uwanja wa Estadio da Luz na atakuwa
chaguo la kwanza baada ya kuondoka kwa mlindamlango Jan Oblak aliyejiunga na
Atletico Madrid.
Cesar ambaye alijiunga na QPR msimu wa 2012 ametumia nusu ya msimu uliopita akicheza kwa
mkopo katika timu ya Toronto ya Marekani kabla ya kuitumikia timu ya taifa ya
Brazil kwenye fainali za mwaka huu za kombe la dunia.
Raia huyo wa Brazil aliyecheza michezo
27 akiwa na QPR timu ya Benfica ni klabu
yake ya nne kuichezea katika hitoria yake ya soka baada ya kuzitumikia Flamengo na Inter Milan ya Italia.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment