Tuesday, August 19, 2014
MOURINHO:NAHITAJI CECH AENDELEE KUBAKI DARAJANI.
Petr Cech.
Kocha wa timu ya Chelsea Jose Mourinho amesema anataka mlinda mlango Petr Cech aendelee kubaki Stanford Bridge licha ya kumpanga Thibaut Courtois katika mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya England ambapo Chelsea ilishinda magoli 3 kwa 1 dhidi ya Barnley jana usiku.
Courtos mwenye umri wa miaka 22 amerejea Chelsea baada ya kucheza kwa mkopo wa miaka mitatu ndani ya mabingwa wa ligi kuu ya Hispania Atletico Madrid na ujio wake umefanya amweke benchi Cech ambaye alikuwa chaguo la kwanza.
Cech mwenye umri wa miaka 32 tangu awasili Chelsea mwaka 2004 alikuwa chaguo la kwanza na ujio wa Courtois umemfanya awe kwenye wakati mgumu kiasi cha kufikiria kuondoka lakini Mourinho amesistiza raia huyo wa jamhuri ya Cech bado anamhitaji.
Mourinho amesema tayari ameshaongea na Cech juu ya hali halisi ilivyo hivi sasa klabuni hapo licha ya mlinda mlango huyo kutofurahia amemweleza kwamba anapaswa kukuliana nayo kwakuwa soka ndivyo lilivyo.
Thibaut Courtois chaguo la kwanza la sasa kwa Jose Mourinho.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment