David Ginola.
Mchezaji wa
zamani wa timu ya taifa ya ufaransa David Ginola ametangaza nia ya kugombea
kiti cha uraisi kwenye shirikisho la soka duniani FIFA akipambana na raisi wa
sasa sepp blatter katika uchaguzi unaotaraji kufanyika baadae mwaka huu.
Nyota huyo alikua balozi wa
uingereza wakati ikiwania kuwa mwenyeji wa fainali za kombe la dunia 2018
ameomba kuungwa mkono na shirikisho la soka barani ulaya na vyama vitano vya
mashirikisho ya soka.
Ginola ambaye alivichezea
vilabu vya Newcastle utd,tottenham hotspurs na everton mwaka 2002,anataraji kukutana na waandishi wa
habari leo jijini London.
Wakati
huohuo makamu wa raisi wa fifa Ali Bin Al Hussein,pamoja na Jerome champagne
ambao kwa pamoja walijiunga na FIFA mwaka 1999,wanataraji kutangaza kuingia kwenye
kinyang’anyiro hicho.
Blatter
amekuwa raisi wa FIFA tangu mwaka 1998 na sasa anawania kugombea kwa msimu wa
tano lakini wagombea kadhaa wamejitokeza kupambana nae kwenye uchaguzi ujao.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment