Nahodha wa timu ya taifa ya Sweden na PSG ya Ufaransa Zlatan Ibrahimovic amepinga
mitazamo ya wachambuzi wa soka kuwa mchezo wa kesho baina ya timu yake ya taifa
na Ureno utakuwa ni kumshindanisha yeye
na Cristiano Ronaldo.
Zlatan amesema mchezo huo unawakutanisha wachezaji wengi kutoka mataifa
mawili kila mmoja akiiwakilisha nchi yake
hivyo wale wanaodhani utawakutanisha yeye na Ronaldo hawako sahihi.
Raia huyo wa Sweden ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa taifa lake na klabu yake
amebainisha umhimu wa mchezo huo ni kuwakutanisha wacheza wengi
wazuri na hilo ndilo jambo ambalo umma
unapaswa kujua.
Sweden na Ureno zinacheza kesho mchezo
maalumu wa kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia na baada ya hapo mataifa hayo yatarudiana tarehe 19 ya mwezi huu mshindi
atakayepatikana atakuwa amekata tiketi ya kwenda Brazil mwakani.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment