Uongozi wa mabingwa wa ligi kuu ya
soka Tanzania bara Yanga umekanusha taarifa za kumsainisha mkataba aliyekuwa kocha
wa Azam fc Stewart Hall na kumfuta kazi
kocha wao Arne Brandts kama ambavyo
baadhi ya vyombo vya habari vilivyoarifu.
Msemaji wa Yanga Baraka kizunguto
amesema kuwa kocha mkuu wa Yanga Arne
Brandts ameenda mapumziko na anatarji kurudi nchini tarehe 24 ya mwezi huu
kwaajili ya kuanza mazoezi ya kujiandaa na duru ya
pili ya ligi kuu.
Kizunguto amesema hata suala la Yanga kumsajili Juma Kaseja ni
mapendekezo yake na pia juu usajili mwingine wa kikosi hicho utakuwa ukilenga
mapendekezo ya wachezaji ambao anawahitaji.
Aidha msemaji huyo amesema
hawajafanya mazungumzo yeyote na aliyekuwa kocha wa Azam fc Stewart Hall kama
ambayoimeripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari huku akitoa ushauri wa bure kwa wanahabari
kuandika habari za ukweli na sio kuidangavya jamii.
Hivi
karibuni kumekuwa na uvumi kwamba Yanga imeachana na kocha wake na ipo kwenye
mipango ya kumsainisha mkataba Stewart Hall ambaye ameifundisha Azam kwa
mafanikio makubwa na sasa amekatisha mkataba wa kuifundisha timu hiyo.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment