Mlinda
mlango aliyetemwa na Simba kisha kukaa
miezi kadhaa bila timu Juma Kaseja amesaini mkataba wa miaka miwili na mabingwa
wa ligi kuu ya soka Tanzania bara klabu ya Yanga yenye makao makuu yake jijini
Dare-salaam.
Kaseja ambaye anatajwa kuwa miongoni mwa magolikipa
bora kuwahi kutokea nchini baada ya
Mohamedi Mwameja “TANZANIA ONE” na wengineo ninavyoona mimi ni kwamba uamuzi wa Yanga kusajili Kaseja unasura kuu mbili ama tatu kwa
wanaolijua vyema soka la Tanzania na vibweka vyake.
1.Kuisaidia
Yanga ambayo imefanikiwa kumaliza duru ya kwanza ya VPL licha ya kuanza vibara msimu huu.
Naamini
Kaseja ni mchezaji ambaye Simba walifanya
kosa kubwa kumtema wakati wakijua
kabisa nyota huyo ambaye anarekodi nzuri
ya kuichezea timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars michezo mingi tangu aanze
kuitwa miaka aliachwa kwa chuki za watu wa chache wenye sauti ndani ya
Simba.Kitendo cha kuachwa na Simba kilimsikitisha kila mpenzi wa Simba ama
shabiki wa timu hiyo lakini kwakuwa wao ni waongeaji wa magengeni haikusaidia
Kaseja arudi tena msimbazi.
Kuona
hivyo macho na masikio yangu yalibaki
yakisubiri kuona dhahabu hii ni nani wa kuiokota au hapa naomba nitumie neon Mvinyo huu ni
nani wa kuununua anayehitaji kupata ladha nzuri na yakipekee.Sikushangazwa na
uamuzi wa kocha wa timu ya taifa ya Tanzania taifa Stars Kim Poulsen kutomwita
kwenye kikosi kinachojiandaa na michuano ya Challenge naamini alifanya hivyo kiprofesheno.
Wenzetu Ulaya
usipocheza kwenye kikosi cha kwanza kwenye klabu yako unahatihati ya
kutoichezea timu ya taifa lako hii tumeiona kwa wachezaji wengi kama Demba Ba ambaye ameshindwa kuitwa kwenye
kikosi cha Senegal licha ya kuwa ni mzuri na kutokuwa chaguo la kwanza ndani ya
klabu yake ya Chelsea mambo yamekuwa hivyo.
Nirudi kwa
kaseja,Naamini Yanga imelamba dume kwakumpata Kaseja na sintoshangaa tena kuona anakuwa golikipa
namba moja na kuwaacha midomo wazi waliomkejeli na kumuona hafai.Kweli ukikiona
cha nini wenzio wanajiuliza watakipata lini,hatimae Yanga wanakila sababu ya
kujivunia kumpata Kaseja.
Miaka miwili
aliyosaibni Yanga Kaseja ataendelea
kuijenga heshima yake kwakuwa najua
atakuwa na Yanga katika michuano ya klabu bingwa Afrika na atawasaidia wakimtumia vyema.
Angalizo
langu ni kwa wale wenye imani za
kishirikina kwamba ukiona mtu flani amewekwa benchi unahoji nakuingiza imani za
kishirikina kwamba si unaona si unaona,tuachane na imani hizo haiwezekani kocha
akamweka benchi mchezaji mwenye nidhamu na uwezo mzuri mambo ambayo binafsi
naamini huwasaidia wachezaji wengi duniani.
Sikushangaa
kuona Casilas akikalishwa benchi na Mourinho ndani ya Ral Madrid kwa mooja ya
sababu nilizozitaja hapo juu hivyo sintoshangaa kuona Kaseja akiwekwa benchi Yanga ka uwezo wake utashuka au akimweka mtu
benchi endapo ataonekana ni bora zaidi yao.
Usikose kufuatilia
sababu zingine ambazo naamini kwanini Yanga
imeamua kumsajili Juma Kaseja.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment