Kiungo mchezeshaji wa klabu ya
Manchester City ya nchini England David Silva anataraji kukaa nje ya uwanja kwa
mwezi mmoja kutokana na kusumbuliwa na
maumivu ya misuli kwenye kigimbi cha mguu.
Raia huyo wa Hispania anakadiriwa kuwa atakosa michezo mitano ya
klabu yake huku akitarajiwa kurudi dimbani tarehe saba ya mwezi ujao ambapo
Manchester City itakuwa ikicheza na Southampton katika ligi kuu ya England.
Silva mwenye umri wa miaka 27 amefunga magoli 3
katika michezo 7 ya ligi kuu ya nchini England.
Pamoja na kumkosa David Silva kwenye
michezo ya hivi karibuni kocha wa timu hiyo Manuel Pellegrin anamatumani makubwa kwamba nahodha Vicent Kompany atakuwepo
katika mchezo baina yao na Tottenham hotspurs nov 24 baada ya kukaa nje ya
uwanja tangu mwanzoni mwa mwezi uliopita
akisumbuliwa na maumivu ya nyama za
paja.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment