Mkongwe wa
Manchester United Ryan Giggs amesema kikosi cha Arsenal kinastahili
kuongooza ligi hadi hivi sasa lakini akisistiza kuwa United bado wanauwezo
mkubwa wa kushinda taji la ligi kuu ya nchini England kwa mara ya 21.
Arsenal
ambayo inaongoza ligi kwa alama 28 ikiwa ni tofauti ya alama 4 na timu
inayoifuatia huku Manchester United ikihitaji alama 9 kukaa juu yake bado Gigis
anamatumaini makubwa ya kutetea ubingwa wao msimu huu wa 2013/2014.
Giggis
amekiri kuwa matokeo mabaya waliyoyapata kwenye michezo 10 ya mwanzo wa ligi
ndiyo yaliyosababisha kufika hapo walipo hivi sasa huku akiongeza kuwa kila
mchezaji wa Man United hajafurahishwa na michezo waliyocheza hadi sasa.
Manchester United ambayo mchezo wake
unaofuata katika ligi kuu ya England inakutana na Tottenham Hotspurs bado Giggis anamaani kikosi chao kitarudi kwenye ubora uliozoelka
kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa 2013.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment