Mshambuliaji wa timu ya Manchester
City inayoshiriki ligi kuu ya nchini England Sergio Aguero amekanusha vikali taarifa zilizovuja kuwa
amefikia makubaliano na Real Madrid kwaajili ya kujiunga nayo mwezi januari
mwakani.
Raia huyo wa Argentina ambaye
amekuwa msaada mkubwa kwenye safu ya ushambuliaji ya kikosi cha City pia ameinyooshea kidole Real Madrid akisema kamwe hana mpango wa kujiunga nao.
Aguero maarufu kama “Kuni”
amebainisha kuwa ukweli ni kwamba anajisikia furaha na maisha ya Manchester na anahudumiwa vizuri na timu tofauti na
akiwa Hispania au Argentina taifa alilozaliwa.
Aguero alijiunga na Manchester City
akitokea Atletico Madrid mwaka 2011 kwa uhamisho wa paundi milioni 35 na
kwasasa amekuwa kwenye kiwango kizuri chini ya kocha wa Manchester City Manuel
Pellegrini.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment