Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 14, 2013

HOFU YA USALAMA YAILAZIMU GHANA KUTUMA UJUMBE MAALUMU NCHINI MISRI KUELEKEA MCHEZO WA MARUDIANO KUFUZU KOMBE LA DUNIA BAINA YA MATAIFA HAYO.



Shirikisho la soka la Ghana  G.F.A limeendelea kuomba ulinzi zaidi kwa nchini ya Misri juu ya timu yao ya taifa itakapocheza mchezo wa marudiano kufuzu fainali za mwakani  za kombe la dunia baina ya mataifa hayo mawili.
Ujumbe  wa watu wanne  kutoka shirikisho la soka  nchini Ghana jana umewasili nchini Misri kwaajili ya kufanya mazungumzo ya pamoja ya kuimarisha usalama kwenye mchezo huo unaotaraji kuchezwa juma lijalo.
Mjumbe wa bodi ya shirikisho la soka nchini Misri Ehab Laheita aliyehudhuria kikao hicho amethibitisha kufanyika kwa mazungumzo nakusema ujumbe wa Ghana umeomba timu yao na mashabiki wake kupatiwa ulinzi zaidi.
Ujumbe wa Ghana umeongozwa na rais wa shirikisho la soka nchini humo Kwesi Nyantakyi,Abedi Ayew Pele,Alhaji Saeed Lartey  ambaye ni afisa usalama wa taifa hilo  pamoja na msemaji wa F.A ya Ghana Ibrahim Sannie.

Posted by Yusuph Mkule.

No comments:

Post a Comment