Kocha wa klabu ya Victoria Pilsen Pavel Vrba
anatarajiwa kuanza kuifundisha timu ya taifa ya Jamhuri ya Czech mwezi januari
mwakani baada ya shirikisho la soka
nchini humo FACR kuthibitisha kwa kutoa tangazo.
Rais wa shirikisho hilo Miroslav Pelta
amebainisha kuwa kazi kubwa ya Pavel
Vrba itakuwa ni kuanza kuiandaa timu yao
kwaajili ya michezo ya mchujo wa kombe la mataifa ya Ulaya 2016 na mkataba wake utaenda hadi mwezi juni mwaka 2015.
Kwaupande wao uongozi wa Victoria Pilsen
umesema kuwa wamekubaliana na uamuzi wa Vrba ambaye ameona ni vyema kutafuta
changamoto mpya za maisha na ataondoka
tarehe 15 mwezi ujao.
Tangu awasili kwenye timu ya Victoria Pilsen
mwaka 2008 Vrba ameshinda mataji
mawili ya ligi na kuiwezesha kucheza
michuano ya klabu bingwa Ulaya ikiwemo
na msimu huu.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment