Timu ya
taifa ya Zanzibar Zanziba Heros imeanza vyema mashindano ya kombe la Challenge
yaliyoanza leo nchini Kenya baada ya kuifunga Sudani kusini magoli 2 kwa 1.
Mchezo huo wa kwanza
wa mashindano hayo yanayoshirikisha nchini wanachama wa Cecafa magoli ya
Zanzibar heros kwenye pambano hilo
lililohudhudhuriwa na watazamaji wachache yamefungwa na Suleiman
Kassim ‘Selembe’ dkk 7 huku lile la pili
likifungwa na Adeyoum Saleh Ahmed katika dkk 67.
Bao la kufutia machozi kwa Sudani kusini limepatikana dkk
73 likifungwa na Fabiano Lako.
Kikosi cha Zanzibar kilikuwa kama ifuatavyo;- Abdallah
Rashid, Salum Khamis/Ally Khan dk78, Waziri Salum, Shaffi Hassan, Mohamed
Fakhi, Sabri Ali, Masoud Ali, Suleiman Kassim, Awadh Juma na Khamis Mcha/Amour
Omar dk44/Adeyoum Saleh dk62.
kikosi cha Sudan Kusini kilikuwa kikiongozwa na ;- Juma Jinaro, Atar Thomas, Philip Delfino, Edomon Amadeo, Richard Justin, Wiiam Offiri, Jimmy Erasto, Thomas Jacob, Godfrey Peter, Francis Khamis/Fabiano Lako dk68 na James Joseph.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment