Kikosi cha Kilimanjaro Stars
kimeaagwa leo na kukabidhiwa bendera ya taifa tayari kwa safari ya
kuelekea Nairobi, Kenya kushiriki michuano ya Kombe la Chalenji inayoanza
kutimua vumbi Novemba 27 mwaka huu.
Stars ambayo imeondoka leo majira ya
saa 10 alasiri kwa ndege ya RwandAir kabla ya kuondoka kocha mkuu wa timu
hiyo Kim Poulsen amewataka wachezaji
kutambua kuwa taifa linawatengemea huku yeye akionyesha matumaini yake kwa
kikosi hicho.
Akizungumza na wachezaji
Katibu Mkuu wa Baraz la michezo la taifa Henry Lihaya amewaomba wachezaji
wa Kili Stars waendeleze nidhamu yao katika mashindano hayo.
Hafla ya kuiaga timu hiyo
imefanyika saa 5 asubuhi kambini kwao katika hoteli ya Accomondia jijini Dar es
Salaam. Msafara wa Kilimanjaro Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium
Lager umeongozwa na Ahmed Idd Mgoyi. Timu imeondoka saa 10 alasiri kwa ndege ya
RwandAir.
Wachezaji waliomo katika
msafara huo ni makipa Deogratius Munishi (Yanga), Ivo Mapunda (Gor Mahia,
Kenya) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Himid Mao (Azam),
Ismail Gambo (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Michael Pius (Ruvu Shooting) na
Said Moradi (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba
(Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba),
Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Ramadhan Singano (Simba) na Salum Abubakar
(Azam).
Safu ya ushambuliaji
inaundwa na Elias Maguli (Ruvu Shooting), Faridi Musa (Azam), Joseph Kimwaga
(Azam), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho
Ngasa (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC).
Hata hivyo, washambuliaji
Samata na Ulimwengu watajiunga na timu hiyo jijini Nairobi, Desemba Mosi mwaka
huu wakitokea Lubumbashi ambapo Novemba 30 mwaka huu TP Mazembe itacheza
fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Benchi la Ufundi la timu
hiyo linawajumuisha Kim Poulsen (Kocha Mkuu), Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi),
Juma Pondamali (Kocha wa Makipa), Leopold Tasso (Meneja wa Timu), Dk Mwanandi
Mwankemwa (Daktari wa Timu), Frank Mhonda (mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred
Chimela (Mtunza Vifaa).
Kilimanjaro Stars ambayo
ipo kundi B katika michuano hiyo itacheza mechi yake ya kwanza Novemba 28 mwaka
dhidi ya Zambia kwenye Uwanja wa
Machakos.
No comments:
Post a Comment