Chama cha
soka visiwani Zanzibar ZFA kimepokea msaada wa shilingi million tano ambazo
zimetolewa na bodi ya ligi kwa ajili ya kusaidia maandalizi ya timu ya taifa ya
Zanzibar Zanzibar Heroes ambayo itashiriki
michuano ya kombe la challenge iliyopangwa kufanyika nchini Kenya mwishoni mwa
mwezi huu.
Afisa mtendaji wa bodi ya ligi
Sailas Mwakibinga amesema wametoa fedha hizo kwa ZFA zenye lengo la kuendeleza
ushirikiano mzuri uliopo kati ya chama hicho na shirikisho la soka nchini Tff pamoja na bodi hiyo.
Ameongeza kuwa milango ipo wazi kwa
ZFA kushirikana na shirikisho la soka nchini ili kuimarisha mahusiano ya pande
hizo mbili na anamatumaini kuwa uhusiano huo utaimarika zaidi ya kwa manufaa ya
taifa.
Wakati huo huo katibu mkuu wa chama
cha soka visiwani Zanzibar ZFA Salum Hadji Kassim amesema suala la kuachwa
kikosini kwa wachezaji Agrey Moris na Nadir Haroub Ally Canavaro halina uhusiano
wowote na adhabu walizozitangaza baada ya kumalizika kwa michuano ya kombe la
Challenge mwaka jana nchini Uganda.
Ameongeza kuwa suala la kuachwa kwa
mchezaji ni uamuzi wa benchi la ufundi kwakuwa
ndilo linalochagua timu ya taifa.
Posted by Yusuph Mkule.
Uongozi wa timu ya Ashanti Utd umekanusha taarifa za kuwasimamisha baadhi ya wachezaji kwamadai ya kuchukua rushwa wakati wa mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara dhidi ya Simba ambao walichomoza na ushindi wa mabao 4 kwa 2.
Msemaji Ashanti Utd Rajab Marijan
amesema wanashangazwa na baadhi ya vyombo vya habari kuvumisha taarifa za
kusimamishwa kwa wachezaji wao nakuongeza
kuwa uongozi ndio wenye mamlaka ya kutoa taarifa zote za klabu.
Amesema hakuna mchezaji awa
wachezaji ambao wamesimamishwa kwa tuhuma za kupokea rushwa na wachezaji wao
wote wapo tayari kwaajili ya duru ya mwisho ya ligi kuu ya soka Tanzania.
Aidha Marijan amekanusha taarifa
zingine ambazo zinawahusisha baadhi ya viongozi wa timu yao ambao wanadaiwa walihusika katika kuuza mchezo
wao dhidi ya Simba kwakusema hakuna jambo kama hilo ambalo limezungumzwa na
baadhi ya vyombo vya habari nchini.
Posted by Yusuph Mkule.
KAMATI YA UTENDAJI YA CHAMA CHA MPIRA MKOA WA RUVUMA KUKUTANA LEO.
Kamati ya utendaji ya chama cha mpira mkoa wa Ruvuma "FARU" leo inakutana kwaajili ya kujadili masuala mbalimbali ikiwemo ligi ya mkoa huo.
Kamati ya utendaji ya chama cha mpira mkoa wa Ruvuma "FARU" leo inakutana kwaajili ya kujadili masuala mbalimbali ikiwemo ligi ya mkoa huo.
Mwenyekiti
wa chama hicho Golden Sanga amesema mmoja ya ajenda itakauwa kujadili ligi ya
mkoa ambayo inataanza mara baada ya wilaya zote za mkoa huo kumaliza ligi zao.
Amesema kikao hicho kinatarajikutoa
na tarehe ya kuanza kwa ligi hiyo ambapo
hadi hivi sasa bado muda wa timu kuchukua fomu za ushiriki unaendelea baada ya
kusogeza mbele mchakato huo kutoka noveba 11 iliyokuwa siku ya mwisho
Aidha Sanga
amezungumzia suala la ukarabati wa uwanja wa majimaji ambapo tayari wameshaanza
hatua za awali na wanataraji kukutana na wamiliki wa uwanja huo unaotumiwa na
vilabu vya majimaji na Jkt Mlale.
Amesema
kamati maalumu itakayokutana na wamiliki wa uwanja huo itakuwa chini ya
uenyekiti wake na wanaimani mchakato huo utazaa matunda na wadau wa Ruvuma wasiwe na wasiwasi wa kutazama michezo
ya ligi kwa timu zao kwakuwa itachezwa kwenye dimba la majimaji.
Posted by Yusuph Mkule.
KIBADENI ALONGA BAADA YA KUTIMULIWA SIMBA.
Baada ya kutupiwa virago na Simba aliyekuwa kocha mkuu wa kikosi hicho Abdalaah King Kibadeni hajapata barua yeyeote ya kufukuzwa na taarifa hizo anazisikia kwenye vyombo vya habari pekeee.
Baada ya kutupiwa virago na Simba aliyekuwa kocha mkuu wa kikosi hicho Abdalaah King Kibadeni hajapata barua yeyeote ya kufukuzwa na taarifa hizo anazisikia kwenye vyombo vya habari pekeee.
Kibadeni
mbali na kuonyesha kusikitishwa kwake na njia ya kuachishwa kazi Simba amelaani
kitendo cha baadhi ya vyombo vya habari kutafsiri kufukuzwa kwake wakifananisha
na kupewa talaka akisema ni kauli za uzalilishaji.
Amesema alitegemea
busara zilizotumika kumleta samba kutoka Kagera Sukari timu aliyokuwa
akiifundisha ndizo zingetumika na si kama walivyo mfanyia.
Hata hivyo
kocha huyo aliyewahi kuichezea Simba kwa mafanikio makubwa amewakosoa waliowaengua
yeye na benchi lake la ufundi kwa kutotumia busara kwakutowapatia burua ya
kuvunja mikataba yao.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment