Kocha mkuu wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho
amesistiza kuwa nyota wa timu hiyo raia
wa Brazil Ramires hauzwi kwa bei yeyote mwezi januari mwakani wakati wa dirisha
dogo la usajili barani Ulaya.
Ramires mwenye umri wa miaka 26 kwa majuma kadhaa yaliyopita amekuwa
akiwindwa na vilabu vya Real Madrid na
mabingwa wa La liga klabu ya Fc Barcelona lakini kauli ya Mourinho inamaanisha ndoto za vilabu hivyo kumsajili mbrazil huyo
zitakuwa zimeota mbawa.
Aidha Mourinho ameongeza kuwa mchezaji
Thibaut Courtois naye hatouzwa kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari
vinavyoarifu kwamba mchezaji huyo anayeidakia Atletico Madrid kwa mkopo atajiunga na timu hiyo kwa mkataba wa kudumu.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment