Shirikisho la riadha nchini RT limepokea
hundi ya shilingi milioni 3 kutoka toka mfuko wa taifa wa hifadhi ya
jamii(NSSF) mkoa wa Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya riadha
yanayoratajia kufanyika mwakani.
Kaimu meneja wa NSSF mkoa wa
Morogoro Mrisho Mwisimba amesema mfuko huo umetoa kiasi hicho cha pesa kwa
ajili ya kuunga mkono jitihada za kuendelea mchezo huo.
Raisi wa shirikisho la riadha nchini
Anthon Mtaka mara baada ya kupokea hundi hiyo amesema kuna haja kwa wanamichezo kujiunga na
mifuko ya jamii kwa ajili ya kuwasaidia pale wanapostaafu.
Aidha Mtaka amewakumbusha
wanamichezo kujiunga na mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamiii ili kunufaika
baadae.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment