TIMU ya soka Future Young Taifa Stars jioni ya leo imeifunga timu ya kwanza taifa , Taifa Stars
goli 1-0 katika mchezo maalum wa
kirafiki uliochezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Goli pekee la vijana hao limefungwa na mshambuliaji wa Ruvu Shooting ya mkoani Pwani, Elias Maguri aliyeunganisha mpira krosi kutoka kwa kinda wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Juma Luizio ambaye alimpokonya mpira mlinzi wa Yanga Kevin Yondan.
Katika mchezo huo Future young taifa Stars imeonyesha kandanda
safi na la kuvutia.
Kipa Ivo Mapunda wa Gor
Mahia ya Kenya alipewa nafasi kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Barthez lango
la Stars na akadaka dakika 45 zote bila kuruhusu bao licha ya Future taifa
stars kushambulia kwa wingi.
Baada ya mechi, kocha wa
Stars, Kim Poulsen ameeleza kuvutiwa kwake na uwezo wa mlindamlango Ivo Mapunda na kwa ujumla mechi hiyo imemsaidia
katika mkakati wake wa kuunda kikosi imara cha kudumu.
Rais mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi alikuwepo Uwanja wa Karume na baada ya mechi alizungumza na wachezaji akiwataka wafanye kazi nzuri ili wafurahie matunda ya uongozi wake.
Aidha Malinzi amewaambia wachezaji wa Stars kuwa
Novemba 19 watacheza na Kenya, Harambee Stars, mchezo wa kirafiki Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam. Rais mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi alikuwepo Uwanja wa Karume na baada ya mechi alizungumza na wachezaji akiwataka wafanye kazi nzuri ili wafurahie matunda ya uongozi wake.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment