Kocha wa
timu ya Sunderland inayoshiriki ligi kuu
ya England Gus Poyet amepewa ruhusa na uongozi wa klabu hiyo kusajili wachezaji mwezi wa kwanza mwakani ili kuimarisha kikosi
hicho.
Poyet ambaye
alichukua nafasi ya Paolo Di Canio
anampango wa kusajili wachezaji watano mhimu watakaosaidiana na waliyopo
ili kuipa nguvu timu hiyo inayoshika nafasi ya kumi na tisa katika msimamo wa
ligi kuu ya England msimu huu.
Timu hiyo
maarufu kama paka weusi inahitajika kushinda michezo mitatu ili iukimbie mstari
wa kushuka daraja kutokana na kuwa na alama saba pekee huku ikishinda michezo
miwili kati ya kumi na mmoja iliyocheza.
Katika
mchezo wake wa hivi karibuni timu hiyo iliifunga Manchester City goli 1 kwa 0 na
juma lijalo inakabiliwa na mchezo dhidi ya Stock City kabla ya kucheza
na Aston Villa na baadae Chelsea kwenye uwanja wake wa nyumbani.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment