Hii ni kati
ya timu ambazo zimewafurahisha mashabiki wa soka si mkoani Mbeya pekee bali
Tanzania nzima.
Soka la
uhakika,kujiamini ni mmoja ya sababu kubwa iliyowafanya wajizolee mashabiki
wengi kila wanapokanyaga katika ardhi ya mkoa wowote hapa Tanzania wakiongozwa na kocha
mzoefu Juma Mwambusi.
Sikushangaa
kusikia mashabiki wao ni wakorofi ,wahuni au vinginevyo nadhani hii
ilinikumbusha usemi usemao mti wenye matunda ndio hupigwa mawe.
Ni kweli
mchezo wa soka umetawaliwa na nidhamu kuanzia nje hadi ndani ya uwanja lakini
si kila mtu amekamilika chakuwaomba mashabiki wa Mbeya City waishangilie timu yao popote na kwa style
yeyote bila kuvuruga amani yasije yakawakuta yaliyowakuta Simba.
Swali ninalojiuliza
ni je, Simba, Yanga, Azam, Coastal Union na Kagera Sukari watakubali kupelekwa
puta duru ijayo au kuna mipango ya kuibomboa Mbeya City wasiendelee kuadhiriwa na
kikosi hichi chenye kiu ya mafanikio?
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment