Pages

Ads 468x60px

Saturday, November 16, 2013

MAKALA.



Na    Issa Maeda.


      Huenda hili ndio kengeza langu.

Mapacha watatu wanoshabihiana kwa sifa bainifu timu ya taifa ya england , bafana bafana na ndugu yao taifa stars', kwaheshima tutaanza na watawala wetu huenda wao ndio walioturithisha ujinga huu kwa fikra zangu england wanaongoza kwa visingizio kila baada ya mashindano fulani baada ya kutolewa kwenye kombe la mataifa ya ulaya 2004 walimlaum sana jorge andrade kwa kuwafanya wafute ndoto yao ya kutwaa kombe la mataifa ya ulaya baada ya kumuumiza mguu nyota wao shujaa wao mwenye umri mdogo wayne rooney kwenye mchezo wa robo fainali ya kombe la mataifa ya ulaya lililoandaliwa nchini ureno hivyo england alitolewa na wenyeji kisha wakapata sababu ya kuongelea kwenye media house, 2006 wakapata nafasi kushiriki kombe la dunia lillilofanyika nchini ujerumani lakini walipokutana na ureno england walipata tena sababu nyingine ya kutoka kwenye michuano baada cr7, kuonekana ndio sababu ya wao kutolewa kwenye michuano kisa alimshtakia rooney kwa refa baada ya rooney kumchezea vibaya ricardo calvaro na rooney akapewa kadi nyekundu na mwisho wa siku ureno walipita england wakirejea nyumbani na kisingizio cha ronaldo walimchukia na walitishia kumuua, 2008 hawakuwa na jipya fainali za euro walizisikia tu ila 2010 walirejea tena safari hii walikutana na kisanga kikubwa mbele ya timu ya taifa ya ujerumani england walizidiwa kila idara mesut ozil tomas muller waliwakimbiza simba watatu mwisho wa siku england alifungwa 4 kwa 1 na kutolewa kwenye mashindano kisingozio kikabaki refa alikataa goli la lampard wakawashawishi wananchi waamini kama goli la lampard lingekubaliwa wangevuka kizingiti cha ujerumani hawakuishia hapo wakawashawishi fifa kuangalia uwezekano wa kuleta goal line technology ilikuondoa utata wa magoli kama la lampard, nahisi wakitolewa kwenye robo fainali ya kombe la dunia 2014 watakuja na sababu nyingine itakayoleta mjadala pia wanaweza kutumia sababu ya kushindwa kumtumia mchezaji flani kama ngao yao ya kujilinda na maadui usishangae wakakwambia hatujasonga mbele kisa januzaj kakataa kuichezea england, leo wamenifurahisha wanaunda kamati itakayoisaidia england itwae kombe la dunia 2022 nchini qatar nawaunga mkono kwa asilimia 100 kwa mpango mkakati huu ila wasisahau kuwa wao hawana vipaji ila wanaweza kutumia njia au sera moja wapo iliyotumiwa na wakoloni wa kifaransa kuwatawala waafrika asimilation kupata vipaji kutoka mataifa yaliobarikiwa ili kuijenga timu ya taifa ya simba watatu, afrika kusini wanatumia sana vyombo vya habari kujitangaza lakini mara ya mwisho kuwaona kwenye kiwango bora ni ule mwaka 1996 walipotwaa kombe la mataifa ya afrika wakiwa na nyota kama lukas radebe, piere issa, dr khumalo adreas arenze wengine kibao baada ya hapo wamekuwa waandaaji wa makombe ila imebaki ndoto kwenye kuyachukua afrika kusini wanaligi bora kama ilivyo england ligi ya afrika kusini ni ya tano kwa utajiri lakini wachezaji wengi wenye vipaji wanatoka nje ya nchi yao hivyo bafanabafana wataendelea kuwa wanyonge kutokana na sera mbovu za shirikisho la soka la nchi hiyo waangalie wapi wanajikwaa ili kuweza kuondokana na uozo kwenye timu ya taifa, wiki iliyopita kocha wa timu ya taifa ya tanzania kim paulsen aliviita vikosi viwili vya taifa stars kimoja cha zamani na future taifa stars kilichonishangaza alimwita golkipa ivo mapunda kwenye kikosi cha future taifa stars hahaha blaza anaumri unaozidi miaka 40 ni vipi atakuwa future au tegemeo la baadae kwenye taifa ambalo mara ya mwisho tulicheza fainali za kombe la mataifa ya afrika mwaka 1980, leo unakiita kibabu kiwe future tunataka future ipi ambayo sio ya kina dilunga, sio ya kina paul nonga, ambayo sio ya kina aishi manula, sio ya kina msuva? Kama ivo ni future tumrejeshe nsajigwa kutoka kwenye kustaafu aje awe future yetu, najiuliza mbeya city ya juma mwambusi na master mind maka mwaluisi hawana mchezaji anayeweza kuisaidia stars kwenye hiyo future, waliwezaje kushika nafasi ya 3 kwenye ligi waliwezaje kutoruhusu kutofungwa magoli mengi waliwezaje kuwa moja ya timu zizoshindikana kufungwa mzunguko wa kwanza, inamaana mbeya city haina nyota angalau wawili kuisaidia future? lakini ghafla usingizi inaniruka na kumbukumbu zinanirejea kuwa pamoja na kuwa na mkurugenzi wa ufundi pale tff hana uzalendo na taifa hili leseni yake ya fifa haitusaidii kuondokana na matatizo yetu, tutabadilisha sana makocha hata tukimpa arsene wenger taifa stars itaendelea kuwa bichwa la mwenda wazimu kwakuwa hatujajua kinachotula kipo nguoni mwetu, mkurugenzi hamtembezi kocha mikoani kujua wachezaji wapya hakuna sera za kuendeleza vipaji kuanzia kata tarafa hadi taifa, tutaishia kulaumiana tu, kama walivyoamka leo england tukaechini tujue tatizo letu nn kisha tutatue mapema ss na afrika kusini na england tuna matatizo yanayofanana, huenda tunaligi bora ila wachezaji wazawa hawana ubora, pia hatuna njia mbadala ya kuzalisha vipaji vipya, au vinavyozalishwa havina muendelezo mzuri,. Tukishindwa tuanzishe kombe letu tuwe tunashiriki tanzania england na afrika kusini labda tunaweza kupata mshindi.

Posted by Yusuph Mkule.

No comments:

Post a Comment