Mshambuliaji wa PSG na nahodha wa timu ya
taifa ya Sweden Zlatan Ibrahimovic ameeleza masikitiko yake kwa taifa lake
kushindwa kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia zitakazofanyika mwakani
nchini Brazil.
Akizungumza baada ya timu yake ya taifa
kunyukwa magoli 3 kwa 2 na Ureno kwenye ardhi yao ya nyumbani Ibra amesema
kwanza anaipongeza Ureno kwa kupata nafasi hiyo ambayo wote walikuwa
wakiiwania.
Zlatan ambaye ameshiriki fainali za kombe la
dunia mara mbili tuu katika historia yake ya soka fainali za 2002 na za 2006
ameiambia tovuti ya Uefa kuwa sababu kubwa ya wao kutolewa na Ureno ni kutokana
na kikosi cha Ureno kuwa bora zaidi yao.
Sweden ambayo imetolewa kwa uwiano wa magoli
4 kwa 2 na Ureno nahodha wao amesema wanapaswa kutazama makosa waliyoyafanya
lakini katika soka lolote laweza kutokea na kuongeza kuwa wamefungwa kutokana
na makosa waliyoyatenda.
Katika mchezo wa jana ambao ulikuwa kama
kipimo cha Zlatan na Ronaldo mreno huyo ameonyesha ubora wake baada ya kufunga
magoli yte matatu kwenye pambano hilo huku Zlatan akiifungia Sweden magoli yao
mawili.
Mbali na Ureno mataifa mengine ya Ulaya yaliyofuzu fainali zijazo za kombe la dunia
hapo jana ni Ufaransa ambayo iliifunga Ukrain magoli 3 kewa 0,Ugiriki iliyopita
kwa uwiano wa magoli 4 kwa 2 dhidi ya Roamania kufuatia kutoka sare ya goli 1
kwa 1.
Croatia pia imefuzu fainali hizo baada ya
kuiadhibu Iceland magoli 2 kwa 0.
BARANI
AFRIKA.
Ghana yenyewe hapo jana imejipatia tiketi ya
kwenda Brazil licha ya kunyukwa magoli 2 kwa 1 na mafarao wa Misri mchezo ulichezwa na kupatiwa ulinzi mkali wa
askari waliokuwa wametanda kila kona.
Mbweha wa jangwani Algeria wakajipatia tiketi
ya kwenda Brazil baada ya kuibuka na ushindi wa goli 1 kwa 0 mbele ya Burkinafaso
na kukamilisha mataifa matano ya Afrika yatakayoshiriki fainali hizo.
Mataifa 32 yaliyofuzu kwa fainali hizo mwakani kutoka kila bara ni kama ifuatavyo.
Kutoka Afrika ni Nigeria,Ivory coast,Cameroon,Ghana na Algeria.
Asia: Australia, Iran, Japan, South Korea
Ulaya : Belgium, Bosnia-Hercegovina, Croatia, England, France, Germany, Greece, Italy, Netherlands, Portugal, Russia, Switzerland, Spain
Amerika ya kaskazini na Caribbean: Costa Rica, Honduras, United States
America kusini: Argentina, (wenyeji) Brazil, Colombia, Ecuador, Chile.
Kutoka Afrika ni Nigeria,Ivory coast,Cameroon,Ghana na Algeria.
Asia: Australia, Iran, Japan, South Korea
Ulaya : Belgium, Bosnia-Hercegovina, Croatia, England, France, Germany, Greece, Italy, Netherlands, Portugal, Russia, Switzerland, Spain
Amerika ya kaskazini na Caribbean: Costa Rica, Honduras, United States
America kusini: Argentina, (wenyeji) Brazil, Colombia, Ecuador, Chile.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment