Shirikisho la soka
kwa nchi za ukanda wa Afrika ya mashariki na kati Cecafa limetangaza makudi ya
timu zitakazoshiriki michuano ya Cecafa Challage Cup inayotaraji kuanza
kuungruma nchini Kenya kuanzia Novemba 27
mwaka huu.
Makundi hayo yamepangwa katika droo maalumu
iliyofanyika nchini Kenya ambapo
wenyeji Harambe Stars wametupwa katika
kundi A
Tanzania bara “Kilimanjaro stars”ikiwa katika kundi B na kundi la tatu yani kundi C linaongozwa na Uganda the Creans.
Katika michuano hiyo mchezo wa ufunguzi
baina ya wenyeji Harambe stars na Ethiopia itachzwa kwenye uwanja wa
Nyayo Stadium novemba 27.
Makundi ya michuano hiyo ni kama
ifuatavyo hapa chini;-
Group A: Kenya, Ethiopia, Zanzibar, South Sudan
Group B: Tanzania, Zambia, Burundi, Somalia
Group C: Uganda, Rwanda, Sudan, Eritrea
Kwamujibu wa taarifa iliyotolewa na
Cecafa mzunguko wa kwanza michezo itachezwa kwenye uwanja wa Nyayo
michezo mingine itakuwa ikichezwa kwenye mji wa Machakosi .
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment