Timu ya soka ya Liverpool
inayoshiriki ligi kuu ya England imetangaza nia ya kutaka kumtoa kwa mkopo
mchezaji wake Rahim Sterling mwezi
januari mwakani lakini ni hadi wapate mchezaji mwenye uzoefu kuziba nafasi
yake.
Kwamujibu wa chanzo kimoja cha habari
barani Ulaya Liverpool imeanza mipango ya kumsajili nyota wa Sporting Lisbon ya
Ureno Diego Capel na endapo wakiridhishwa nae watamchukua kama mbadala wa
Sterling ambaye ni raia wa England.
Mwanzoni mwa juma hili kocha wa Liverpool
Brendan Rodgers alibainisha kwamba Sterling ni mchezaji ambaye anatakiwa
kupambana zaidi ili aweze kuwa kwenye kikosi cha kwanza cha majogoo hao wa Anfield.
Kwamsimu uliopita Rahim alionyesha uwezo
mkubwa baada ya kuichezea Liverpool michezo
36 na kisha kuitwa kwa mara ya kwanza
kwenye timu ya taifa ya England.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment