Kiungo wa klabu ya soka ya Fc Barcelona Cesc
Fabrigas ameanza mazoezi baada ya kuendelea kupona vyema jeraha lake la goti
lililokuwa linamsumbua uongozi wa timu hiyo umethibitisha.
Mchezaji huyo jana mchana alianza mazoezi
jana mchana na kushiriki vipindi
vyote taarifa ya klabu hiyo ambayo ni mabingwa wa ligi kuu ya
Hispania imeeleza.
Aidha Barcelona kupitia tovuti yake imesema
kuwa walinzi Gerard Pique na Jordi Alba wanaendelea na mazoezi ya pamoja na
wenzao baada ya kuendelea vyema kutokana na
majeruha yaliyokuwa yakiwasumbua.
Fabrigas alimia goti la mguu wa kushoto
kwenye mchezo ambao Barcelona ilishinda magoli 4 kwa 1 dhidi ya Real Betis
mapema mwezi huu katika mchezo wa ligi kuu
jambo lililomfanya aondolewe kwenye kikosi cha timu ya taifa ya
Hispania.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment